Maana
Muhugo ni aina mojawapo ya zao la nafaka. Muhogo hutokana na mzizi lakini pia majani yake yanalika kama kisamvu.
Viinilishe katika Muhogo
Muhogo una kiasi kikubwa sana cha wanga (uthibitisho unahitajika) ukilinganisha na nafaka nyingine.
Matumizi
Mbali na kutumika kama chakula muhogo hutumika kutengenezea madawa, vifungashio na katika viwanda vya nguo na n.k.
Faida za kulima muhogo
Tofauti na nafaka nyingine muhogo unaweza kustahimili ukame na kukua vizuri katika udogo usio na rutuba(uthibitisho unahitajika).
Vikwazo katika kilimo cha muhogo
Katika nchi zinazoendelea wakulima wa muhogo wanakumbwa na vikwazo vifuatavyo:
- Mbegu duni.
- Ujuzi duni.
- Uhifadhi duni.
- Wadudu waharibifu.
- Magonjwa.