Chakula ni kitu ambacho watu ama wanyama wanakula na mimea inafyonza ili kuleta na kuwezesha uhai.

Hivyo chakula ni lishe. Afya bora inatokana na mpangilio mzuri wa ulaji wa chakula. Hapa ni muhimu kuzingatia uwiano mzuri wa makundi ya vyakula na muda wa milo.

Mara nyingi watu katika nchi zinazoendelea wanakumbwa na matatizo yanayosababishwa na ulaji wa chakula usiozingatia mpangilio ama uwiano mzuri wa makundi ya vyakula. Lakini hii inasababishwa na umaskini, njaa hasa inayosababishwa na hali mbaya ya hewa na ukame na miundombinu mibovu.

Katika nchi zinazoendelea watoto wengi na wazee wanaonekana kuwa na utapiamlo. Ukijionesha kupitia unyafuzi na kwashakoo.

Ukurasa huu ni kipisi tafadhali saidia kuendeleza!

Cookies help us deliver our services. By using our services, you agree to our use of cookies.