Teknohama ni dhana ya jumla inayotilia mkazo mawasiliano ya pamoja na muingiliano wa mifumo ya mawasiliano(mikonga ya simu na mawimbi upepo/wireless signals), ujenzi wa mifumo imara ya usimamizi na mifumo ya sauti-picha katika teknolojia ya habari ya kisasa. Teknohama, yaani ICT inajumuisha mahitaji yote ya kiufundi kuwezesha habari na kusaidia mawasiliano, ikijumuisha kompyuta na vifaa vya mfumo mgumu, mfumo wa kati wa mawasiliano na mfumo laini unaohitajika. Tunaweza sema ICT inajumuisha matumizi ya simu, vyombo vya kurusha matangazo/habari, aina zote za kuchakachukua na kurusha sauti na picha na miundo ya mitandao ya usimamizi na ufuatiliaji.