Voltimita ni kifaa kinachotumika kupima volti katika sakiti ya umeme. Ili kupima volti, voltimita huwekwa sambamba na sehemu ama chombo kinachoitajika kupimwa volti zake. Volti zinaweza kuweka katika moja ya elfu moja, yaani mV, moja mara, yaani 1×V, 10×V n.k. Lakini katika siku za usoni voltimita zinashindwa umaarufu na maltimita na zinaanza kupotea ama kupatikana kwa shida. Hii ni kwa sababu maltimita inafanya kazi nyingi zaidi, kwa mfano kupima kiasi cha mkondo wa umeme, kapasitensi na volti.