Tafsiri
Mpunga ni aina ya nafaka ambayo baada ya kukobolewa hutoa mchele. Mchele ni chakula maarufu sana hasa katika bara la Asia.
Matumizi
Matumizi makubwa ya mpunga ni pamoja na chakula yaani, mchele, malisho ya wanyama, kutoa nishati joto, mboji toka katika mabaki n.k kutegemeana na eneo husika.
Viinilishe
Mpunga/mchele huna viinilishe vya wanga kwa kiasi kikubwa na protini kidogo na mafuta katika kiwango kidogo sana.
Kilimo cha mpunga
Mpunga hustawi katika maeneo ya mabondeni kwenye udongo hunaotuamisha maji na joto kali (uthibitisho unahitajika). Hivyo mpunga hulimwa zaidi katika maeneo yenye hali ya kitropiki.