Chakula ni kitu ambacho watu ama wanyama walasha na liverpool

inafyonza ili kuleta na kuwezesha uhai.

Hivyo chakula ni lishe. Afya bora inatokana na mpangilio mzuri wa ulaji wa chakula. Hapa ni muhimu kuzingatia uwiano mzuri wa makundi ya vyakula na muda wa milo.

Mara nyingi watu katika nchi zinazoendelea wanakumbwa na matatizo yanayosababishwa na ulaji wa chakula usiozingatia mpangilio ama uwiano mzuri wa makundi ya vyakula. Lakini hii inasababishwa na umaskini, njaa hasa inayosababishwa na hali mbaya ya hewa na ukame na miundombinu mibovu.

Katika nchi zinazoendelea watoto wengi na wazee wanaonekana kuwa na utapiamlo. Ukijionesha kupitia unyafuzi na kwashakoo.

Umuhimu wa chakula[edit | edit source]

Tunakula chakula ili kuondoa njaa na kuupa mwili virutubisho vya kuufanya uendelee kuwa na nguvu na afya bora. Chakula lazima kiwe safi na salama na kinatakiwa kiwe cha kutosha kulingana na umri, kazi na hali ya mtu. Ubora wa chakula pia hutegemea upatikanaji wa virutubisho vyote, yaani wanga, protini, mafuta, maji, madini na vitamini.

Madhara ya lishe duni[edit | edit source]

Madhara yafuatayo husababishwa na kutokuzingatia lishe bora.

  • Utapiamlo.
  • Kiriba tumbo.
  • Unyafuzi.
  • Kwashakoo.

Unyafuzi[edit | edit source]

Unyafuzi husababishwa na ukosefu wa virutubisho vya aina ya protini kama mayai, nyama n.k.

Dalili[edit | edit source]

  • Kupungua uzito.
  • Nywele za rangi ya shaba na dhaifu.
  • Tumbo kubwa.
  • Kuvimba kwa uso na miguu.
  • Kukosa hamu ya kula.

Nyongea[edit | edit source]

Nyongea husababishwa na kukosekana kwa wanga na mafuta ya kutosha katika chakula.

Dalili[edit | edit source]

  • Upungufu mkubwa wa uzito.
  • Kuzeeka kwa sura.
  • Kwa watoto hutaka kula wakati wote.
  • Macho meupe.

Kiribatumbo[edit | edit source]

Kiribatumbo husababishwa na kuzidi mafuta mwilini. Kiribatumbo huambatana na maradhi kama vile ugonjwa wa moyo na shinikizo la damu.

Rovu[edit | edit source]

Rovu husababishwa na ukosefu wa madini joto/iodine mwilini. Rovu hujitokeza kwa kuvimba tezi za shingo. Pia kudumaa kwa akili na mwili hutokea.

Upungufu wa damu[edit | edit source]

Upungufu wa damu ama uwekundu wa damu husabisha udhaifu wa mwili, kuchoka mara kwa mara, kusinzia na kuhema haraka haraka. Tatizo hili usababishwa na upungufu wa madini chuma.

Kwashakoo[edit | edit source]

Kwashakoo husababishwa na ukosefu wa protini mwilini.

Dalili[edit | edit source]

  • Kuvimba tumbo.
  • Nywele laini zenye rangi ya shaba/nyekundu.
  • Ngozi mbaya iliyopasukapasuka.
  • Kuvimba kwa ini.
  • Upungufu wa damu.

Usomaji zaidi[edit | edit source]

http://en.wikipedia.org/wiki/Food

Ukurasa huu ni kipisi tafadhali saidia kuendeleza!

FA info icon.svg Angle down icon.svg Page data
Authors Christopher Sam
License CC-BY-SA-3.0
Derivative of Food
Language Kiswahili (sw)
Related 0 subpages, 7 pages link here
Impact 4,083 page views
Created Mei 5, 2011 by Christopher Sam
Modified Aprili 13, 2024 by Kathy Nativi
Cookies help us deliver our services. By using our services, you agree to our use of cookies.